Historia ya Cristiano Ronaldo akizaliwa Huko Madeira Ureno na Maisha yake ya soka.

Cristiano Ronaldo ni mchezaji wa soka barani ulaya, ambae ameweka historia kubwa ya mchezo huo katika kiwango bora kabisa. Alizaliwa huko Funchal, Ureno mnamo mwaka 1985, tangu utotoni mwake, alionyesha vipaji vya kipekee katika uwanja wa mpira. Baada ya kuanza kazi yake na sporting Lisbon, alipata umaarufu mkubwa alipojiunga na Manchester United mwaka 2003.

Akiwa na Manchester United, Ronaldo aliimarisha jina lake kama mmoja wa wachezaji wenye vipaji vya juu Zaidi katika soka la Ulaya na ulimwenguni kwa ujumla.Aliisadia klabu hiyo kushinda mataji kadhaa, ikiwa ni Pamoja na ligi kuu ya England na ligi ya Mabingwa UEFA,mafanikio  yake yalimfanya apate tuzo ya Mchezaji bora wa Dunia FIFA mwaka 2008.

Baadae alihamia klabu ya Real Madrid kwa Ada ya Paundi million 80 akivunja rekodi ya usajali kwa mwaka huo wa 2009, akiwa ndiye mchezaji aliepata ada kubwa ya uhamisho mwaka  huo. Kuhamia kwake Real Madrid mwaka wa 2009 kulikuwa hatua muhimu katika kazi yake ya soka. Huko, alikuwa mchezaji muhimu katika klabu hiyo, akishinda taji la Ligi ya Mabingwa ya UEFA mara nne na kuvunja rekodi nyingi za ufungaji wa mabao.Ronaldo alitunukiwa Tuzo ya mchezaji bora wa Dunia ya FIFA mara nne Zaidi akiwa na Real Madrid, akiifungia klabu hiyo mabao 450 ikiwa ni recoki ya juu mno kuwa kufikiwa na historia ya wachezaji wa klabu hiyo ya Los blancos.

Mwaka 2018, Ronaldo alihamia katika klabu ya Juventus, ambapo aliendelea kufanya vizuri nakuwa nguzo muhimu ya kikosi hicho. Aidha, amekuwa mchezaji muhimu katika timu yake ya Taifa ya Ureno, akishinda mataji muhimu kam vile UEFA Euro 2016 na UEFA Nations League mwaka wa 2019.

Mwaka 2021 alihamia katika klabu yake ya zamani ya Manchester United akiibuka mfungaji bora wa klabu hiyo, kabla yakukumbwa na msimu mbaya mwaka 2022, hali iliyomfanya avunje mkataba na klabu yake hiyo, na kutimkia Uarabuni katika klabu ya Alnasr nchini Saudi Arabia.

Kwa ujumla Cristiano Ronaldo amejipatia umaarufu na heshima kubwa katika ulimwengu wa soka kupitia uwezo wake wakipekee wakupachika mabao na mafanikio yake ya klabu na timu ya Taifa. Yeye ni mmoja wa wachezaji bora katika mchezo huo wa mpira wa miguu na anasalia kuwa kielelezocha mafanikio na juhudi kwa kwa wachezaji wengi duniani kote, akitamba na aina yake yaushangiliaji wa magoali iliyopachikwa kwa jina la SIUUUUU na mashabiki wake ulimwenguni huku ikiendelea kuigwa na wachezaji wa kizazi kipya kama Rodrigo mchezaji namba 11 wa Real Madrid.

Cristiano Ronaldo kwa Sasa anakipiga huko al-nasr ya uarabuni saudia, na ameibuka Kama mfungaji Bora wa msimu huu wa 2023/24, nakufanikiwa kuwa mchezaji wa kwanza kutwaa kiatuujumla.Aliisadia Cha ufungaji Bora akiwa na umri wa miaka 39...ikiwa ni tofauti kabisa na wachezaji wengine walio wahi kutokea katika mchezo wa soka.

Na Sasa anajiandaa kikamilifu kukipiga katika mashindano ya Euro 2024, yatakayo anza kutumia vumbi huko nchini Ujeruman kwenye majira ya joto June 16 mwaka wa alfu mbili na ishirini na nne, akiwa amevaa jezi ya ureno kama mchezaji mkongwe na mzoefu wa mashindano hayo...akifanikiwa kuonekana katika mashindano hayo mara Tano mfululizo.

Na pia amejikita katika uwekezaji wa Mahoteli ya kifahali katika majiji mbali mbali huko barani Ulaya na Africa. Na mwaka 2023 alihusika katika kushiriki shughuli za kijamii nchini Morroco alipotoa moja ya hoteli yake iliyopo nchini humo Kama sehemu ya kuhifadhi watu kufuatia tetemeko la Ardhi lililo ipiga nchi hiyo.

Cristiano Ronaldo alimaarufu Kama CR7,..Amekuwa akizaminiwa nakutumiwa katika kuwasilisha matangazo ya kampuni kubwa ya kibiashara na inayojihusisha na utengenezaji wa jezi za mpira (NIKE), ambayo imekuwa ikimbunia mtindo wa viatu vyake vya kuchezea soka.