Farida Mohammad Kabir

edit

Farida Mohammad Kabir (aliyezaliwa 25 Julai 1992) ni mtaalamu wa magonjwa wa Nigeria, msanidi programu, na mjasiriamali wa teknolojia na pia ndiye kiongozi wa timu ya Google Women TechMakers na mratibu mwenza wa Google Developer Group, Abuja. Farida Mohammad Kabir pia ndiye mwanzilishi/Mkurugenzi Mtendaji wa OTRAC, kampuni ya teknolojia ya afya ambayo inatengeneza mifumo ya biashara ya sekta ya afya nchini Nigeria. [1]

Maisha na Elimu

edit

Farida Kabir alizaliwa London, Uingereza, mwaka wa 1992. [2] Yeye ndiye mkubwa kati ya mabinti watano katika famia yao. Kabir lisoma shule ya msingi huko Lagos na shule ya upili huko Kaduna Nigeria. Baada ya kumaliza elimu ya msingi Alijiunga na elimu ya juu katika Chuo Kikuu cha Ahmadu Bello Ahmadu Bello University,zaria nchini Nigeria kuanzia Januari 2009 hadi Aprili 2014, na kuhitimu Shahada ya Sayansi katika Sayansi ya Biolojia. [4] Mnamo mwaka wa 2015, alijiungana mafunzo ya kuwa mtaalamu wa mbele wa magonjwa ya kuambukiza na Mpango wa Mafunzo ya Epidemiolojia na mafunzo ya Maabara ya NCDC. Baadaye Baadaye alipata udhamini kutoka kwa Taasisi ya Visiola ili kusoma maendeleo ya programu za komputya. Kabir pia ana shahada ya MBA kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa la Benki ya Dunia. [3]